Ally H. Laay

Ally H. Laay

Mwenyekiti wa Bodi

Bw Laay ajiunga nasi kwa utendaji wake usio na shaka na bora kabisa kutoka Kamati ya Ukaguzi Mahesabu ya SAGCOT, ambapo amekuwa na mjumbe hai wa Kamati hii. Uzoefu wake kwenye tathmini ya miradi ya uwekezaji kwenye Chai, Kahawa, Maziwa na Pamba ambayo wafadhili mbalimbali wanaongezea thamani. Uzoefu wake mpana na wa muda mrefu katika maisha yake huanzia kutoka: Benki ya Kilimo ya china, kwa miradi husila inayofadhiliwa na ODA & DANIDA na Wizara ya Kilimo, Ushirika na Maendeleo ya Mifugo kama Afisa kiongozi mwenye jukumu la kuandaa Taarifa ya Mambo na Tathmini ya Uhai wa Vyama vya Ushirika vya mikoa ya Tabora na Shinyanga vilivyoko Eneo la Magharibi la Uzalishaji Pamba (jina linalojulikana kama WCGA chini ya DANIDA). Kwa sasa, Bw. Laay ni Mjumbe wa Bodi katika taasisi zifuatazo: Benki ya CRDB Plc, ambapo ni Mwenyekiti wa Bodi, Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC). Bw. Laay ni mhitimu wa Shahada ya Uzamili ya Uongozi wa Biashara kutoka Skuli ya ha Biashara - Chuo Kikuu cha Wales (Uingereza), Diploma ya Uzamili ya Uhasibu kutoka Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Mhasibu Mwenza wa Umma Aliyeidhinishwa (FCPA (T).