“Ni safari yenye mafanikio. Asante, Geoffrey pamoja na wafanyakazi wote wa Taasisi ya SAGCOT (SCL) kwa kuniandalia na kunipa fursa ya kuwatembelea wabia wenu walioko mkoani Iringa. Nimefurahishwa sana kuona namna ya ukaribu uliopo kati ya Serikali na sekta binafsi, kuanzia ngazi ya mkoa mpaka kwenye ngazi ya jamii. Hongereni Taasisi ya SAGCOT kwa kazi nzuri”

“Ukweli nimefurahishwa na kazi inayofanywa na Taasisi ya SAGCOT (SCL) na wabia wake. Ninaguswa sana na hali ya uwajibikaji iliyopo ambayo ni chachu ya kuongeza na kupanua mafanikio haya tuliyopata. Nilifahamu, sio tu mafanikio yenu na uwezo zaidi ambao upo ndani ya njia ya utekelezaji wa SAGCOT lakini pia changamoto ambazo Tanzania inakabiliana nazo na namna inavyojiandaa kuleta mafanikio kwenye kilimo biashara, kama sehemu muhimu ya “ukuaji wa Viwanda”. Kwa hivyo basi hii imekuwa ikiniangazia sana. Tulipambana sana kupata idhini ya SAGCOT na tutaendelea kukipigania kituo hiki kwa ajili ya siku zijazo. Na pia kuangalia ni jinsi gani tunaweza kutumia nguvu za ziada ili kuimarisha mafanikio ambayo tayari tunayapata”

“Kazi ya Taasisi ya SAGCOT imetupatia ufahamu mzuri juu ya upana, utofauti na uwezo wa wabia wa SAGCOT. Ilishangaza kuona kwamba wabia wameazimia na kuhakikisha kuwa wanarudisha sehemu ya faida wanayopata kwa jamii zilizopo kwenye maeneo wanakoendesha miradi yao, kwa kuanzisha fursa za uzalishaji vipato (ajira), kuwawezesha wakulima wadogo kupata masoko ya mazao yao, na kusaidia upatikanaji wa riziki kwa majirani wa karibu kupitia uanzishaji wa programu za mafunzo na warsha za ushauri wa kitaalam n.k. Ni ukweli ulio wazi kabisa kuwa Taasisi ya SAGCOT kinajijengea heshima, ambayo kwa kiasi kikubwa imetokana na njia ambayo kituo kinatumia kutekeleza kazi zake kwa utulivu, utashi mkubwa na jumuishi ambayo inakubalika na kufuatwa na wadau walioko kwenye ukanda, tangu awali. Nakuomba uendelee kuisimamia kazi hii nzuri unayofanya wewe pamoja na wafanyakazi wote wa Taasisi ya SAGCOT. Hakuna swali kwa namna tulivyofurahishwa kwa yale tuliyoyaona, na tunatazamia kuendelea kuimarisha ubia wa SAGCOT kwa kipindi cha miezi na miaka ijayo”

“Ziara yangu ya kikazi pale Kongani ya Ihemi wakati ulipokuwa unafanyika Mkutano Mkuu wa mwaka ilinipatia uzoefu mkubwa sana. Nilipata fursa ya kukutana na wabia wenzangu wa Taasisi ya SAGCOT (SCL) walioko ndani ya ubia yakiwemo mabenki, Mfuko wa Kuchochea Maendeleo ya Kilimo wa SAGCOT, wasambazaji/wauza mbolea na taasisi tofauti za fedha waliohudhuria mkutano huo. Nashukuru kwa namna ambavyo ubia miongoni mwa wadau una thamani na pia una umuhimu mkubwa kwa wakulima wadogo kama mimi. Kwa sasa ninawasiliana na mabenki ambayo wameonyesha nia ya kushirikiana nami kupitia mradi wangu.”
“Tumeonyesha namna sekta ya umma na binafsi, watendaji wasio wa kiserikali na washirika wa maendeleo, wanavyoweza kufanya kazi pamoja katika njia bunifu na wakafanikia kukuza na kutekeleza miradi ya uwekezaji jumuishi na wajibifu katika kilimo”
“Nikiwa kama Waziri mwenye mwenye dhamana na wajibu wa kusimamia Kilimo; nimeridhishwa na kupongeza kazi inayofanywa na Taasisi ya SAGCOT katika Ukanda wa Kilimo Nyanda za Juu Kusini. Mipango ya Taasisi ya SAGCOT inaenda sambamba na kile ambacho wizara inakipigia debe katika jitihada zinazotuelekeza kufanikisha usalama wa chakula nchini. “Njia ya SAGCOT” itasaidia kufanikisha utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II). ”
“Mafanikio ya ubia uliopo ambao Taasisi ya SAGCOT kinatoa msaada, wakulima wadogo na washirika wa kibiashara kwenye mnyororo wa thamani wa vipaumbele katika Kongani zote, na wabia wote wanategemeana kwa pamoja. Kwa hiyo, tunawaalika wawekezaji wote wenye wajibu wa kuwekeza katika ukanda wetu, kutoa ajira, na kuwasaidia wakulima wadogo”

“Kwa niaba ya Wakala wa Maendeleo ya Wakulima Wadogo wa Chai Tanzania (TSHTDA), Nampongeza Bw. Geoffrey Kirenga kwa kuandaa safari hii ya kihistoria. Safari hii ya kujifunza imepanua uelewa na ufahamu kwa wengi, sio tu Wabunge bali kwa watanzania wote kwa ujumla, juu ya ukweli kuhusu maendeleo ya zao la chai nchini. Hii inahusu hasa, ukitazama ubia kati ya serikali na sekta binafsi kwenye Mradi wa Njombe.  Asanteni !”