Image

Karibuni kwenye Ukanda wa Kilimo kusini mwa Tanzania

Mpango wa Kukuza Kilimo Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (“SAGCOT”) ni Mpango wa Ubia kati ya Serikali na Sekta binafsi uliozinduliwa wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Uchumi Duniani ulipofayika Dar-es-Salaam mwaka 2010.
 
Utekelezaji wake unachukua kipindi cha miaka 20 mpaka mwaka 2030. Lengo kuu ni kuongeza tija ya uzalishaji kwenye kilimo, kuimarisha usalama wa chakula, kupunguza umaskini na kuhakikisha uhifadhi endelevu wa mazingira kupitia urasimishaji wa kibiashara kwa wakulima wadogo. Jukumu la ubia huu ni kufikia lengo hili la kuchochea maendeleo ya kilimo yanayoongozwa na sekta binafsi ndani ya mazingira ya biashara yanayoboreshwa kila mara.
 

Utaratibu wa Utekelezaji wa Mpango wa SAGCOT

Mpango wa SAGCOT unatekelezwa kupitia Kongani. Kongani ni eneo la kijiografia lenye mkusanyiko wa wadau kwenye minyororo mbalimbali ya thamani. Msingi wa Kongani ni kuonyesha mwingiliano wa kazi za wadau katika eneno husika na mahusiano yaliyopo ili kufanikisha maendeleo ya biashara. Taasisi ya SAGCOT kinafanya kazi ya uwakala mwaminifu wa kuunganisha Wabia kusaidia kazi zao kuwa na ufanisi. Ubia wa SAGCOT unashirikisha makampuni ya kilimo biashara, asasi za wakulima, asasi za kiraia, na wakala mbalimbali wa serikali wakipewa jukumu la pamoja la kuendeleza minyororo ya thamani iliyopewa vipaumbele kwenye miradi ya kilimo. Hivyo, wabia hufanya kazi kutatua vikwazo walivyobaini kwa pamoja.

Aina za ubia zimegawanyika kulingana na minyororo ya thamani ambapo kuna minyororo 9 ya thamani; Soya, Chai, Maziwa, Nyanya, Viazi mviringo, Miwa, Mpunga, Parachichi na Alizeti.

 
Image
Image
Image

Mazingira ya Ubia wa SAGCOT

Ubia wa SAGCOT unaongozwa na kanuni zifuatazo:

 Kuwashirikisha wakulima wadogo na kuhakikisha wanazingatia uhifadhi       endelevu wa mazingira kwa shughuli wanazofanya;

 Kushirikiana na wabia wengine ili kukuza njia inayowaunganisha na       kuboresha jitihada za pamoja ndani ya minyororo ya vipaumbele ya       thamani;

 Kudumisha ushiriki, mawasiliano na msaada kwa Taasisi ya SAGCOT;

 Kuchangia kwenye utatuzi wa vikwazo vya kisera na miundombinu; na

 Kuchochea ubunifu kwenye utatuzi wa changamoto zikiwemo za kifedha.

Unaweza kuuelezea Mpango wa SAGCOT kama ndoto inayotelezeka. Utekelezai wa ndoto au maono hayo unatokanana na kuwepo Mikakati ya Utekelzaji wa Mpango wa SAGCOT inayotekelezwa kwenye vipindi vya miaka mitano-mitano. Mikakati hiyo, hutumiwa kuandaa mipango kazi ya kila mwaka na kuweka mfumo wa kitaasis ya kuratibu na kutathmini utekelezaji kupitia SAGCOT Centre Ltd.

Historia Yetu

Taasisi ya SAGCOT Centre Limited (SCL) kilianzishwa kama kampuni yenye dhamana iliyosajiliwa kisheria mnano mwaka 2011. Kituo hiki hufanya kazi kama wakala mwaminifu na kichocheo cha ubia miongoni mwa asasi wabia kuhuisha mipango inayohusu minyororo ya thamani jumuishi, endelevu na yakinifu kwenye kilimo. Jukumu kubwa la Taasisi ya SAGCOT ni kuwezesha wabia ili kutekeleza kazi za minyororo ya thamani jumuishi, endelevu na yenye faida kibiashara kwenye kilimo katika Ukanda wa SAGCOT. Kituo hiki ni kiunganishi cha watendaji walioko kwenye mfumo mzima wa kiikolojia. Majukumu ya Kituo ni pamoja na: 

Kutoa taarifa zinazohusu uwekezaji wa sekta binafsi na umma, fursa   zilizopo ndani ya ubia, na maboresho kwenye vipaumbele vya sera ili kufikia   malengo ya SAGCOT;
Kufuatilia hatua za maendeleo ya utekelezaji, kupitia zoezi la ufuatiliaji na   tathmini ndani ya ubia, kuhakikisha utekelezaji wa ahadi za wabia na     maendeleo wanayoyapata ili kufikia malengo yao;
Kuhimiza na kuwezesha ushiriki endelevu wa sekta binafsi katika kukuza     ubia imara;
Kuendeleza maboresho ya sera na sheria ambayo ni muhimu katika     kufikia malengo ya SAGCOT;
Kutoa masomo, kutumia njia za upangaji mipango ya Kongani na     uwezeshaji wa wabia, na kuwasiliana kwa niaba ya Ubia wa SAGCOT na;
Kukuza ubia wa SAGCOT, na fursa zilizopo ndani ya ubia, kwa hadhira     pana na kwa safu ya wabia wa kikanda na kimataifa.
Image