Image

Ubia wa Ukanda wa Kukuza Kilimo kusini mwa Tanzania (SAGCOT) una wajibu wa kubadili sekta ya kilimo katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania, kwa kuchochea uwekezaji jumuishi na wenye uhifadhi endelevu wa mazingira. Kufanikisha lengo hili kunahitaji mipango na uwekezaji ambao unajali mali asili za Tanzania, mifumo ya kiikolojia na bio anuai; kuendeleza mifumo ya uzalishaji kilimo yenye faida na shughuli za uendeshaji wa minyororo ya thamani ambayo inazingatia uhifadhi endelevu wa mazingira na inayowajibika kwa jamii, kuwezesha jamii juu ya mbinu za matumizi bora ya mali asili zilizopo na kuchukua tahadhari dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi; kutengeneza fursa za kibiashara kwa wakulima wadogo na jamii ambazo zitaruhusu uzalishaji wa mali endelevu; na unaozingatia sheria na viwango vilivyowekwa kuanzia ngazi ya kijamii, kitaifa na kimataifa.

Kikundi cha Kilimo endelevu na jumuishi/shirikishi cha SAGCOT (GRG) ni jukwaa la wadau mbalimbali wanaofanya kazi kama chombo cha ushauri kisichokuwa rasmi katika Taasisi ya SAGCOT katika ngazi za taifa na kongani. GRG inawashirikisha pamoja kundi la wawakilishi wa wadau kutoka serikalini (Ofisi ya Makamu wa Rais, Wizara za Kilimo, Maliasili na Utalii, Elimu, Ujenzi, Ardhi na Maendeleo ya Makazi), sekta binafsi (ikijumuisha wakulima na makampuni), jumuiya za wafadhili (RNE, UNEP), na asasi za kiraia (WWF, CARE International, TNC, IUCN and AWF), pamoja na washauri binafsi wa masuala ya kisayansi.  SAGCOT GRG ilianzishwa kusaidia Taasisi ya SAGCOT kuratibu na kufuatilia masuala ya kimazingira katika programu zilizoko kwenye Ubia wa SAGCOT. Kimuundo wa utawala, Kikundi cha GRG   kinaongozwa na wenyeviti wenza ambao ni Ofisi ya Makamu wa Rais (inawakilisha Serikali ya Tanzania) na Meza ya Majadiliano ya Maafisa Watendaji Wakuu (CEOrt), inawakilisha sekta binafsi. Katika ngazi ya kongani, Kikundi hiki kinasimamiwa na Katibu Tawala wa Mkoa husika vilevile na wawakilishi kutoka makampuni ya sekta binafsi ndani ya kongani kuhakikisha ajenda ya uendelevu na changamto a katika shughuli zote za kongani za SAGCOT. Wabia wawekezaji wa Sekta za Umma na Binafsi walioko katika kongani sio tu wameungana kwa mujibu wa sheria bali kufanya kazi kwa kufuata sheria zilizoko na pia kuungana kiuweledi kuhimiza ushirikishaji wa wadau kwa namna ambayo ni rafiki kwa mazingira na pia ukuaji wa kilimo endelevu kwa jamii, wakifanya kazi kwa karibu na Taasisi ya SAGCOT. Jitihada hii zinatekelezwa kwa nyenzo ya muhimu inayoitwa Mwongozo wa Ukuaji Shirikishi na Endelevu  (Inclsuive Green Growth au IGG tool) ambayo SAGCOT hutumia kusaidia makampuni madogo mpaka makubwa kuelewa nini maana ya ukuaji shirikishi na endelevu  na namna gani ya kuingiza katika kazi zao za usimamizi.

Lengo la msingi la Kikundi cha GRG   ni kutoa mwongozo, ushauri na mapendekezo kwa Taasisi ya SAGCOT na wabia wake juu ya masuala ya kimazingira na kijamii. Mwongozo huu hujumuisha maendeleo ya fursa za ukuaji endelevu  na kilimo himilivu kwa mabadiliko ya tabia nchi, vilevile utambuzi na kushughulikia kwa pamoja mambo hatarishi na hasara zinazotokana na uharibifu wa mazingira. Pia kukisaidia Taasisi ya SAGCOT kukuza na kuongeza ufahamu juu ya fursa jumuishi zilizoko kwenye ukuaji endelevu .

Ushauri unaotolewa na Kikundi cha GRG   hautoi masharti kwa mbia bali huongozwa na Kanuni ya Kushughulika Mambo Hatarishi, Kanuni ya kumtoza malipo Mharibifu/Mchafuzi wa Mazingira na Kanuni Thabiti za Umoja wa Mataifa zinazosimamia Mazingira. Kusimamia matumizi endelevu na kwa busara mali asili zilizopo na kuhimiza ubunifu kwenye Ukuaji wenye uendelevu. GRG husaidia utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi Mazingira iliyosainiwa mwaka 2004 kwenye mipango endelevu ya muda mrefu (miaka 10-30) kama SAGCOT.

Uanachama wa Kikundi cha Rejea Ukijani huakisi Ubia Shirikishi kati ya Serikali na Sekta Binafsi ambao ni haiba ya SAGCOT. Pia huakisi maslahi tofauti na umahri wa kiufundi vinavyohitajika kusimamia utofauti na ugumu unaojitokeza kwenye uendeshaji. Muundo wa Kikundi Rejea Ukijani umelenga kuwezesha kuwepo na ushiriki mkubwa kwa makundi ya wadau wakuu - Serikali ya Tanzania, jumuiya ya wafadhili, sekta binafsi na asasi za kiraia-huku wakitimiza lengo na kuongeza ufanisi. Wanachama wote ni wabia waliosajiliwa kwenye Ubia wa SAGCOT, ukiondoa wataalamu waliopewa mkataba na Kikundi Rejea Ukijani kutoa huduma mahsusi au utaalamu wao.

Kikundi cha GRG   kimepanga kuhakikisha kinaweza kuleta matokeo kwa wakati uliopangwa, huku wakitoa majibu kwa mahitaji yaliyowasilishwa na Taasisi ya SAGCOT. GRG   kitahakikisha kuwa wataalamu huru wa masuala ya kiufundi na ushauri wa kisayansi wanapatikana muda wowote wanapohitajika na wanachama. Kwa hiyo Taasisi ya SAGCOT kinahitaji wanachama wa GRG   kusambaza taarifa, kuomba ushauri na kupewa maelekezo kutoka jamii pana ya wadau kutoka maeneo wanayotoka. Uanachama katika GRG   uko kwa mwaliko wa Taasisi ya SAGCOT na Sekretarieti. Utoaji maamuzi ndani ya Kikundi hichi  hufanyika kwa msingi wa maridhiano/au makubaliano ya pamoja.

Mnamo mwezi Mei 2016 Kikundi cha GRG kilianza kazi katika ngazi ya Kongani ambapo Kikundi hicho hutoa nyenzo ya kuongoza uwekezaji katika ngazi ya Kongani kwa Wabia wa SAGCOT ndani ya Kongani husika. Kati ya mwezi Mei na Disemba  2022, GRG ilitumia Mwongozo wa IGG ambao huongoza uwekezaji kujitahmini uzingatiaji wa kanuni za uwekezaji shirikishi na endelevu. Jumla ya biashara   41 zimefanyiwa tathmini na kuweka msingi wa kuboresha uendeshaji wa biashara endelevu. vile vile GRG iliandaa Mdahalo wa wadau mtambuka juu ya Matumizi ya Ardhi – mkutano wa ulioshirikisha nchi mbalimbali na kuratibiwa na asasi ya The Forests Dialogue kutoka marakani na kshirikiana pamoja na safu ya wabia wa ndani kwa lengo  kukusanya maarifa na michakato inayowezesha uwajibikaji kibiashara na uwekezaji, kuimarisha utawala, na maendeleo jumuishi kwenye maeneo ya ardhi. Mjadala wa Matumizi ya Ardhi hulenga kuelewa na kuboresha utekelezaji kwa vitendo wa “Njia ya Eneo la Ardhi” ili kushughulikia ushindani wa kimaslahi unaotokea mara kwa mara miongoni mwa wadau tofauti katika eneo husika la ardhi, ambao ni jambo muhimu kwa usimamizi endelevu wa ardhi na kwa ajili ya maendeleo mapana ya kiuchumi na kijamii.