Image
Ifikapo mwaka 2030, wabia wa SAGCOT wanatarajia kuona kuna hekta 350,000 za ardhi zinatumika kwa ajii ya uzalishaji wa kilimo kinacholeta faida za kibiashara, kusaidia kuleta mabadiliko kwa wakulima wadogo 100,000 wanaoendesha kilimo kujikimu sasa hivi kwenda kuwa wakulima wanaoendesha kilimo biashara, kutoa fursa ya ajira kubwa 420,000, kuwainua watu milioni 2 kutoka kwenye umaskini, na kuongeza mapato yanayotokana na uzalishaji bidhaa za kilimo kufikia kiasi cha Dola za Kimarekani bilioni 1.2 kwa mwaka.
Ili kuweza kufanikisha hili, kila Mbia wa SAGCOT ana wajibu wa kuwashirikisha wakulima wadogo kwenye shughuli kilimo biashara na kuhakikisha wanazingatia uhifadhi endelevu wa mazingira; kushirikiana na wadau wengine kukuza njia inayowaunganisha pamoja, kuongeza mshikamano, kudumisha ushiriki, mawasiliano na kusaidia Taasisi ya SAGCOT (SCL), kuchangia kwenye utatuzi wa vikwazo vya kisera na miundombinu, kufikria mbinu mpya na bunifu za usimamizi wa fedha.
SAGCOT hutoa faida nyingi kwa wabia- muhimu zaidi, fursa ya kuleta mabadiliko ya kweli kwa maendeleo ya kilimo na kuwa sehemu ya kipekee, mpango wa kubadili matokeo.

Utekelezaji wa kazi za ubia unafanyika ndani ya kongani; maeneo ya kijiografia yenye mkusanyiko wa wakulima waliothaminiwa wenye mahusiano yanayowaweka pamoja, miradi ya kilimo biashara, watoa huduma wenye uwezo wa kutoa misaada inayoshabihiana (k.m. miundombinu ya usafirishaji, maghala na huduma za kigani) Njia ya kutumia kongani inasaidia watendaji binafsi kuanzisha shughuli za kiuchumi zenye kuleta manufaa kwa jamii na kuimarisha matokeo zinazopatikana.

Wabia wanaunganishwa na dira/maono ya kawaida, utamaduni na imani ili kufikia lengo la muda mrefu ambalo ni ushirikiano utakaosaidia kubadili taswira ya maendeleo ya kilimo nchini Tanzania. Hii hutoa kiungo muhimu kinachohitajika ndani ya ushirikiano wenye mafanikio kati ya taasisi tofauti zinazofanya shughuli anuai za utekelezaji. Utamaduni wa kawaida unaounganisha ubia wa SAGCOT unaopanuka huku ukizingatia Kanuni za Maadili na kuweka Kanuni za Ubia ambazo wabia wote wanapaswa kuzifuata katika kutimiza wajibu wao wa kiutendaji.

Image