Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Mpango wa SAGCOT ni mkutano wa wanachama wote wa taasisi pia ni kikao cha juu cha maamuzi katika hairakia ya mpango. Mkutano Mkuu unajumuisha taasisi tatu waasisi ambazo ni Baraza la Kilimo Tanzania (ACT), Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI). Taasisi hizi ni makampuni yenye hisa katika Mpango wa SAGCOT.

Image
Image
Image

Baraza la Kilimo Tanzania (ACT)

Baraza la Kilimo la Tanzania (ACT) mwamvuli wa Asasi za Sekta Binafsi unaofanya kazi ya ushawishi na utetezi kwa niaba ya wanachama wake katika ngazi ya taifa na ngazi ya chini kuhusu masuala ya sera na mazingira ya biashara yanayoathiri sekta ya kilimo. Lengo la msingi la Baraza la Kilimo Tanzania ni kuunganisha wanachama wote ambao ni jamii ya wakulima na wafugaji nchini Tanzania na kufanya kama chombo cha wanachama katika majadiliano na serikali na vyombo vingine kuhusiana na uundaji na usimamizi wa sera na programu zinazohusika na maendeleo ya kilimo na kilimo biashara nchini. Baraza hili linaundwa na vyama vya wakulima, vyama vya wafugaji, vyama vya ushirika, vyama vya wasambazaji pembejeo, vyama vya wasindikaji wa bidhaa za kilimo, vyama vya wasafirishaji, na watafiti.

Shirikisho la wenye Viwanda Tanzania (CTI)

Shirikisho la Viwanda Tanzania ni Asasi wa Uanachama wa Biashara iliyozinduliwa mwezi Julai 1991. Ni asasi huru, inayojiendesha yenyewe kifedha, asasi iliyosajiliwa kwa mujibu wa sheria kuhudumia wanachama wake kuwa msemaji kwa niaba ya wanachama wake na kuwakilisha maslahi ya wanachama wake kwa ujumla.
Kutokana na kuwepo na mazingira ya biashara yasiyokuwa rafiki miaka ya 1990, Shirikisho la wenye Viwanda lilibaini masuala machache kama kipaumbele kwa kazi ya Utetezi. Mazingira haya yalijumuisha sera za Bajeti na kodi, muundo wa sheria na udhibiti, mipangilio ya mahusiano ya kibiashara za kikanda na nchi nyingine, na miundombinu, hususan Umeme, Barabara, Reli na Bandari.
Lengo kuu la Shirikisho la wenye Viwanda ni kuhakikisha kunakuwepo na mazingira rafiki ya kisheria, kifedha na kiuchumi ambayo yatawezesha viwanda kujiendesha kikamilifu, kustawi na kuchangia kwenye utajiri wa taifa na maendeleo. Shirikisho limekuwa mstari wa mbele katika kutetea uwepo wa mazingira rafiki ya kibiashara kwa wanachama wake ili waweze kuwa na ushindani.  

Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI)

Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) ilianzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Bunge Na. 10 ya mwaka 2016 kukuza na kuimarisha mfumo wa utafiti wa kilimo nchini Tanzania. Tassisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania ina chombo chenye nusu mamlaka chini ya Wizara ya Kilimo kikiwa na wajibu wa kusimamia shughuli zote za utafiti wa kilimo zinazofanywa na Mfumo wa Taifa wa Utafiti wa Kilimo (NARS) nchini Tanzania.
Taasisi ina mamlaka ya kufanya, kudhibiti, kukuza na kuratibu shughuli zote za utafiti wa kilimo zinazofanywa na taasisi au asasi za utafiti za umma na binafsi nchini Tanzania. Taasisi inalenga kuimarisha mfumo wa taifa wa utafiti wa kilimo ili kukuza maendeleo na usambazaji wa teknolojia, ubunifu na mazoea katika usimamizi (TIMPs) kushughulikia mahitaji halisi ya wakulima na wadau wengine wa kilimo.
Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania ina mtandao wa vituo 9 vya utafiti na vituo vidogo 8. Vituo hivyo ni TARI Makutupora, TARI Ilonga, TARI Selian, TARI Ukiriguru, TARI Naliendele, TARI Mlingano, TARI Tumbi, TARI Uyole and TARI Kihinga. Vituo vidogo ni  TARI Hombolo, TARI Dakawa, TARI Maruku, TARI Mikocheni, TARI Tengeru, TARI Kifyulilo, TARI Ifakara and TARI Kibaha. Makao makuu ya Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) yapo jijini Dodoma, Tanzania.